Tanzania kama ilivyokuwa kwa Kenya ilitawala kipindi cha kwanza na kukosa nafasi kadhaa za wazi za kufunga magoli.
Katika dakika ya 65 ya kipindi cha pili Morocco ilizima ndoto za Tanzania kwa holi safi lililofungwa na mshambuliaji Oussama Lamlaoui.
Tanzania ambayo iliongoza kundi B kwa kutinga robo fainali kibabe bila kufungwa hata mechi moja ikashindwa kendeleza ubabe mbele ya Morocco baada ya hapo.
Morocco imetwaa ubingwa wa CHAN mara mbili huku Taifa Stars ikitinga hatua hii kwa mara ya kwanza baada ya kushiriki mara tatu.
Awali Kocha wa Taifa Stars Hemed Suleiman alisema kuelekea mchezo huo "Nimeangalia makundi yote naamini kwamba kila timu katika kundi lolote ni mzuri na inaweza kuleta ushindani. Sisi tupo tayari kukabiliana na Morocco."
Katika hatua ya makundi, Morocco ilikuwa tayari imeshinda mechi tatu na kuchapwa moja dhidi ya Kenya.
Imefunga mabao manane sawa na wastani wa kufunga mabao mawili katika kila mechi na kuruhusu mabao matatu.
No comments:
Post a Comment
Subscribe My YouTube Channel Here:
https://www.youtube.com/channel/UCRdp...
Like My Facebook page:
https://www.facebook.com/lyizzmaker
Follow Me On Twitter:
https://www.twitter.com/habariyamjini
Follow Me on Instagram:
https://www.instagram.com/habariyamjini