Monday 29 August 2016

MATUKIO MANNE KUTIKISA SEPTEMBA MOSI.

Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakiwa katika mazoezi huko Monduli, Arusha. Jeshi hilo litaadhimisha miaka 52 ya kuanzishwa kwake Septemba Mosi kwa kufanya usafi katika mitaa mbalimbali ya nchi.
Tarehe 1 Septemba wiki hii itakuwa siku ya aina yake nchini kutokana na kubeba matukio makubwa manne moja likiwa la kimataifa litakalofanya macho mengi duniani kuelekezwa Tanzania. Matukio hayo ni kupatwa kwa jua kitendo kitakachotokea kwenye usawa wa anga ya Tanzania katika eneo la Rujewa mkoani Mbeya na lile la Waziri Mkuu kuhamia rasmi Dodoma ikiwa ni kutekeleza ahadi yake aliyoitoa mara baada ya Rais John Magufuli kutangaza azma ya Serikali yake kuhamia huko katika kipindi cha miaka minne na ushee ya utawala wake kilichobaki.