Tuesday, 23 September 2025

Tetesi za Soka: CASEMIRO KUMFUATA RONALDO AL-NASSR?



Al-Nassr anayochezea Christiano Ronaldo, wanalenga kumsajili kiungo wa Manchester United, Casemiro, 33, huku mkataba wa Mreno huyo katika Old Trafford ukitarajiwa kumalizika majira ya joto. (Mundo Deportivo)

Manchester United wanapigana vikumbo na Atletico Madrid na Barcelona kumsajili mshambuliaji wa Serbia, Dusan Vlahovic, 25, ambaye mkataba wake huko Juventus unamalizika majira ya joto yajayo. (La Gazzetta dello Sport, via Teamtalk)

Real Madrid wanaonyesha nia ya kumsajili beki wa Tottenham Hotspur, Micky van de Ven, 24, huku klabu hiyo ya kaskazini mwa London ikimthaminisha Mholanzi huyo kwa dau la takriban pauni 70 milioni. (Fichajes)

Inter Miami wako karibu kumpa mkataba mpya wa muda mrefu mshambuliaji wa Argentina, Lionel Messi, 38, aliyesajiliwa kwa mara ya kwanza na klabu hiyo ya MLS mwaka 2023. (ESPN)

No comments:

Post a Comment

Subscribe My YouTube Channel Here:
https://www.youtube.com/channel/UCRdp...

Like My Facebook page:
https://www.facebook.com/lyizzmaker

Follow Me On Twitter:
https://www.twitter.com/habariyamjini

Follow Me on Instagram:
https://www.instagram.com/habariyamjini