Tuesday, 26 August 2025

CHAN 2024: WENYEJI WANA CHAKUJIVUNIA BAADA YA KUTOLEWA?



Wikiendi iliyomaliza, mechi za robo fainali ya African Nations Championship (CHAN 2024) zilichezwa katika majiji manne (Dar es Salaam, Kampala, Nairobi na Zanzibar) katika nchi tatu na timu zote waandaaji, ikiwa na maana Kenya, Tanzania na Uganda zimetolewa katika mashindano hayo.
Kenya imefungishwa virago na Madagascar katika mikwaju ya penalti ya 4-3, katika uwanja wa nyumbani wa Karasani siku ya Ijumaa. Kenya ilianza kwa ushindi wa goli moja, kabla ya goli hilo kurudishwa kwa mkwaju wa penalti, na kushindwa kuongeza goli jingine hadi dakika 90 na 30 za nyongeza.

Tanzania imetolewa na mshindi mara mbili wa kombe hilo Morocco, kutoka Afrika ya Kaskazini, baada ya kufungwa goli moja katika kipindi cha pili katika mechi iliyochezwa siku ya Ijumaa, na kushindwa kurudisha goli hilo katika uwanja wa nyumbani wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam.

Uganda ilifungwa goli moja katika kipindi cha pili mbele ya maelfu ya mashabiki katika uwanja wa Nelson Mandela jijini Kampala siku ya Jumamosi. Robo fainali yao ilikuwa ni dhidi ya bingwa mtetezi Senegal kutoka Afrika Magharibi.

Hatua ya Uganda kucheza robo fainali, ni historia mpya kwa timu hiyo baada ya kushiriki michuano hiyo mara nyingi zaidi kuliko waandaaji wenzake. Kwa maana hiyo Uganda imeondoa gundu walilokuwa nalo kwa miaka mingi.

Fainali za mwaka huu ni za tatu kwa Tanzania kushiriki baada ya kufanya hivyo mwaka 2009 iliposhirika katika kundi 'A' na kuishia makundi, ikimaliza nafasi ya tatu na pointi nne. Tanzania ikashiriki tena mwaka 2020 na kuishia tena makundi, ilipomaliza nafasi ya tatu kundi 'D' na pointi nne.

Timu hiyo imeweka historia mwaka huu, sio tu kwa kucheza fainali kwa mara ya kwanza, pia kushinda michezo yao yote katika makundi na kutoa suluhu mchezo mmoja. Ushindi ambao unaonyesha kukuwa kwa soka la timu hiyo.

Kenya imepata nafasi ya kushiriki michuano ya CHAN 2024 kwa mara ya kwanza, kama mojawapo ya mataifa matatu waandaaji. Wameandika historia ya kufika robo fainali, pia kuifunga Morocco katika makundi, mshindi wa CHAN 2018 na 2020.

No comments:

Post a Comment

Subscribe My YouTube Channel Here:
https://www.youtube.com/channel/UCRdp...

Like My Facebook page:
https://www.facebook.com/lyizzmaker

Follow Me On Twitter:
https://www.twitter.com/habariyamjini

Follow Me on Instagram:
https://www.instagram.com/habariyamjini