Tuesday, 26 August 2025

Uchaguzi Tanzania 2025: FAMILIA TANO ZA VIGOGO CCM ZILIZOPENYA MBIO ZA UBUNGE.


Chama cha Mapinduzi (CCM), moja ya chama kikongwe barani Afrika kinajiandaa na uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, miongoni mwa maandalizi hayo ni kupata wagombea wa nafasi mbalimbali ikiwemo Ubunge, Uwakilishi na Udiwani, huku wakiwa na uhakika kuwa Rais wa sasa wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ndiye mgombea wao katika nafasi ya urais.

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, ilipitisha majina ya watia nia wa nafasi mbalimbali, kwa ajili ya kwenda kupigiwa kura za maoni na wajumbe, kisha majina hayo yakarudi kwa halmashauri kuu ya chama kwa ajili ya kuchagua jina moja.

Mwishoni mwa wiki hii CCM ilitoa orodha ya majina ya watakaogombea Ubunge, wale wa viti maalum na nafasi za baraza la Wawakilishi kwa upande wa Tanzania bara na Zanzibar.

Katika orodha ya wagombea wa CCM, wapo ambao wametoka katika familia za vigogo wa chama hicho, kuanzia rais wa sasa na marais wastaafu, pia wanachama wengine wa ngazi ya juu katika chama hicho.

 

No comments:

Post a Comment

Subscribe My YouTube Channel Here:
https://www.youtube.com/channel/UCRdp...

Like My Facebook page:
https://www.facebook.com/lyizzmaker

Follow Me On Twitter:
https://www.twitter.com/habariyamjini

Follow Me on Instagram:
https://www.instagram.com/habariyamjini