
Maafisa wa afya wa Gaza wamesema shambulizi hilo kwenye hospitali ya Nasser huko Khan Younis liliwauwa watu 20 na kuwajeruhi wengine zaidi ya 80.
Ni miongoni mwa mashambulizi mabaya zaidi ya Israel ambayo yamezikumba hospitali na waandishi wa habari katika vita vilivyodumu kwa miezi 22.
Shambulio hilo lilijiri wakati Israel ikipanga kupanua mashambulizi yake kwenye maeneo yenye wakazi wengi, ikiapa kuwaangamiza Hamas baada ya shambulio lake la Oktoba 7, 2023.
Miongoni mwa waliouawa ni waandishi Habari watano, akiwemo Mariam Dagga, mpiga picha wa shirika la Habari la AP, mwenye umri wa miaka 33. Shirika la Habari la Reuters lilisema mmoja wa maripota wake aliuawa katika shambulizi la mwanzo wakati akipiga picha za moja kwa moja za televisheni kwenye ghorofa ya juu ya hospitali ya Nasser huko Khan Younis.
Waandishi wengine, akiwemo Dagga, na wafanyakazi wa uokozi walikuwa wamevalia vizibao vya chungwa vya huduma za dharura wakati walipolipuliwa katika shambulizi la pili walipokuwa wakipanda ngazi za jengo hilo kwenda kwenye eneo la mkasa.
Israel yasema inachunguza
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ameliita shambulizi hilo kuwa la "bahati mbaya” na kusema jeshi linalichunguza. Alisema Israel inajutia tukio hilo na kwamba inathamini kazi ya waandishi, wahudumu wa afya na raia wote.
Brig. Jen. Effie Defrin, msemaji wa jeshi la Israel, amesema jeshi huwa haliwalengi raia na kwamba limeanzisha uchunguzi wa ndani kuhusu mashambulizi hayo. Aliwahutumu Hamas kwa kujificha miongoni mwa raia lakini hakusema kama Israel iliamini wanamgambo wowote walikuwepo wakati wa mashambulizi kwenye hospitali hiyo.
No comments:
Post a Comment
Subscribe My YouTube Channel Here:
https://www.youtube.com/channel/UCRdp...
Like My Facebook page:
https://www.facebook.com/lyizzmaker
Follow Me On Twitter:
https://www.twitter.com/habariyamjini
Follow Me on Instagram:
https://www.instagram.com/habariyamjini