Iliwalazimu majaji kuahirisha shauri la Mwenyekiti huyo wa CHADEMA kwa saa nzima baada ya mvutano mkali. Hata wanachama wachache wa CHADEMA walioingia kwenye ukumbi wa mahakama hiyo walilazimika kutoka nje baada ya kubaini kuwa wenzao wamezuiwa.
Kesi yaanza kusikilizwa baada ya mashauriano
Majira ya saa 5 asubuhi, kesi ilianza na katika hatua ya usikilizwaji ambapo Lissu atatoa sababu ya pili ya pingamizi lake, kuhusu uhalali wa mahakama hiyo kusikiliza kesi hiyo.
Ufafanuzi huu hata hivyo umepokelewa kwa hoja mchanganyiko, baadhi wakihoji kuhusu uhalali wa polisi kuwapiga raia lakini wengine wameunga mkono hoja ya Muliro.
Lissu amesema hati ya mashitaka dhidi yake ina mapungufu makubwa. Anahoji ni chapisho gani hasa kuhusu matamshi yake linatakiwa liwasilishwe, ama liwe kwa aina ya barua, barua pepe au chapisho jingine na kusisitiza watu wanaodaiwa kupokea taarifa hizo walipaswa kutajwa kisheria, vinginevyo hati hiyo inabaki kuwa na kasoro kubwa isiyoweza kurekebishwa.
No comments:
Post a Comment
Subscribe My YouTube Channel Here:
https://www.youtube.com/channel/UCRdp...
Like My Facebook page:
https://www.facebook.com/lyizzmaker
Follow Me On Twitter:
https://www.twitter.com/habariyamjini
Follow Me on Instagram:
https://www.instagram.com/habariyamjini