Wednesday, 17 September 2025

Tetesi za Soka: MECHI TATU ZIJAZO KUAMUA MUSTAKABALI WA AMORIM MAN UNITED.


Ruben Amorim anakabiliwa na kipindi kigumu kama mkufunzi wa Manchester United, huku mechi tatu zijazo zikiamua iwapo atasalia kuinoa Old Trafford au la. (Daily Express)

Meneja wa Crystal Palace Oliver Glasner, mkufunzi wa zamani wa England Gareth Southgate, mkuu wa Fulham Marco Silva na Iraola wa Bournemouth ni miongoni mwa wanaoweza kuchukua nafasi ya Amorim iwapo Manchester United itamfukuza. (Daily Star)

West Ham pia wameanza kufikiria warithi wa kocha Graham Potter ambaye hana presha na wanataka mtu ambaye anaweza kukichangamsha kikosi na mashabiki wa klabu hiyo. (TeamTalks)

Newcastle wanafikiria kumnunua kiungo wa kati wa Manchester United mwenye umri wa miaka 20 kutoka Uingereza Kobbie Mainoo Januari. (Talksport

Real Madrid na Paris St-Germain wanafuatilia hali ya William Saliba katika klabu ya Arsenal, huku mazungumzo yakiendelea kuhusu mkataba mpya wa beki huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 24. (CaughtOffside)

No comments:

Post a Comment

Subscribe My YouTube Channel Here:
https://www.youtube.com/channel/UCRdp...

Like My Facebook page:
https://www.facebook.com/lyizzmaker

Follow Me On Twitter:
https://www.twitter.com/habariyamjini

Follow Me on Instagram:
https://www.instagram.com/habariyamjini