Kwa zaidi ya robo karne, jina la Maalim Seif Sharif Hamad lilihusiana moja kwa moja na siasa za upinzani Zanzibar. Kwa wafuasi wake, alikuwa alama ya matumaini; kwa wapinzani wake, alikuwa mpinzani sugu, asiyechoka, ambaye mara zote aliamini kuna nafasi ya mabadiliko.
Kila uchaguzi tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi, jina la Maalim Seif lilikuwa katikati ya majukwaa, kura na mijadala ya kisiasa.
Kifo chake mwaka 2021 kimeacha pengo kubwa ambalo uchaguzi wa 2025 unakabiliana nalo kwa mara ya kwanza. Kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1995, Zanzibar inakwenda kwenye uchaguzi mkuu bila kivuli chake kizito. Swali kuu liko wazi: bila Maalim Seif, upinzani una sura gani, na CCM inakutana na changamoto ipi?
Maalim Seif alianza siasa zake ndani ya CCM (wakati huo ASP na baadaye CCM) kabla ya kugombana na chama hicho mwishoni mwa miaka ya 1980. Hapo ndipo alipoanza safari yake ya upinzani kupitia Chama cha Wananchi (CUF), akakijenga kuwa chama kikuu cha siasa visiwani. Baadaye, alihamia ACT-Wazalendo baada ya migogoro ya ndani ya chama chake cha zamani. Katika kila hatua, aliibeba Zanzibar kwenye majukwaa ya siasa za upinzani kitaifa na kimataifa.
No comments:
Post a Comment
Subscribe My YouTube Channel Here:
https://www.youtube.com/channel/UCRdp...
Like My Facebook page:
https://www.facebook.com/lyizzmaker
Follow Me On Twitter:
https://www.twitter.com/habariyamjini
Follow Me on Instagram:
https://www.instagram.com/habariyamjini